,

MARTIN KADINDA ASHINDWA KUFICHA HISIA ZAKE JUU YA JACK PATRICK, AFUNGUKA HAPA

1:17 AM

MWANAMITINDO maarufu Bongo, Martin Kadinda ameonesha hisia zake hadharani baada ya kutupia picha ya rafiki yake kipenzi, modo Jack Patrick mtandaoni na kuonesha kuwa amemkumbuka.

Modo Jack Patrick.
Jack alikamatwa nchini China akidaiwa alikuwa amebeba madawa ya kulevya ambapo kabla hajaondoka, walikuwa wakishirikiana kikazi na mwanamitindo huyo ambaye amemwambia mwandishi wetu kuwa waliishi kama ndugu.
Mwanamitindo maarufu Bongo, Martin Kadinda.
“Jack Patrick alikuwa zaidi ya rafiki, tuliishi vizuri, tumekula good time pamoja na mambo mengine mengi, sitaki kuongelea ishu yake iliyompata lakini kimsingi namkumbuka sana,” alisema Kadinda.

 -GPL

#SHARE THIS NEWS AND WIN!!!#

You Might Also Like

0 comments

JIUNGE UPATE HABARI

Jisajili Sasa upate E-mail ya Kila Tunachochapisha....