Makada
watatu wa CCM akiwemo aliyekuwa mgombea ubunge wa Jimbo la Kibaha Mjini
mwaka 2010, Dk. Rose Nkonyi, wamejiunga na CHADEMA.
Makada hao
walijiunga na CHADEMA jana na kukabidhiwa kadi na Mwenyekiti wa chama
hicho ngazi ya taifa, Freeman Mbowe, katika mkutano wa hadhara
uliofanyika Mailimoja, ikiwa ni ziara ya Operesheni Movement For Change
(M4C) Pamoja Daima.
Waliojiunga
na CHADEMA mbali na Dk. Nkonyi ni Joseph Chakale, aliyekuwa mjumbe wa
Kamati ya Utekelezaji CCM ngazi ya wilaya na Hafidh Mudhihiri aliyekuwa
Katibu wa Vijana wa Tawi la Mailimoja.
Wakizungumza
katika mkutano huo makada hao walisema wameamua kuihama CCM baada ya
kubaini chama hicho hakina dhamira ya kuwaletea Watanzania maendeleo.
#SHARE THIS NEWS AND WIN!!!#
0 comments