Taarifa
ambazo zimetufikia muda Mfupi uliopita zinasema Kuna ajali mbaya ya
Barabarani imetokea Huko karibu na KIA Moshi ajali ambayo imehusisha
Basi Dogo la Abiria aina ya Coaster na Lori la mizigo Aina ya Fuso
ambapo yamegongana uso kwa uso na kusababisha vifo.
Coaster hiyo ilikuwa ikitoak Arusha
kwenda Moshi ikiwa imesheheni Abiria wa kutosha inasemekana ilikuwa
ikienda kwa mwendo kasi na Dereva kushindwa kuhimili kuyumba kwa gari
hilo wakati ambapo akiwa katika mwendo kasi kitu ambacho kilifanya
ashindwe kupishana na Lori hilo lililokuwa likitoka Moshi kwenda Arusha.
Shuhuda wa Ajali hiyo ambaye alikuwa
akitoka Arusha kwenda Moshi ameongea na Haazu na kusema kuwa Kuna
uwezekano kwa watu wachache sana kupona katika Ajali hiyo kwani hata
sura za watu wengi hazijulikani huku Majeruhi wakiwa katika hali mbaya
zaidi.
Kwa upande wa Dereva Shuhuda wetu amesema
kuna uwezekano mkubwa sana kuwa Dereva kafariki hapo hapo kwani upande
wake ndio ulioathiriwa Zaidi.
Shuhuda wetu pia ilikuwa ahusike kwenye
ajali hiyo kwani alilisimamisha gari hilo mara kadhaa ili asafiri nalo
na Dereva hakusimama kitu kilichomlazimu kusubiri gari lingine na
kusafiri nalo na Kufika Karibu na KIA ndipo alipokuta gari hiyo ikiwa
imeisha.
MSIKILIZE HAPA CHINI SHUHUDA AKIONGEA NA HAAZU#SHARE THIS NEWS AND WIN!!!#
0 comments