,

JE, UNAJUA WANAWAKE WAREMBO SANA HUPENDA WANAUME GANI? SOMA HAPA

12:28 AM







Yapo maoni na maswali tofauti  kwenye vichwa vya watu wengi juu ya aina gani hasa ya wanaume hupendwa sana na wanawake warembo na hata wale wakawaida ambao uzuri wao kidogo umefichika. Wapo watu wanafikiri wanaume wenye sura nzuri ndio hupendwa zaidi,wapo baadhi hufikiri wanaume wenye pesa ndio kila kitu,wapo wengine hudhani mwanaume mtanashati na anayepiga pamba ndio habari ya mujini La hasha,Hii si kweli hata kabisa.

Mapenzi nayoyazungumzia hapa si mapenzi yale ya kuigiza,wala si yale yakushawishiwa na kitu flani cha mpito kama vile mavazi au pesa,aku mi si zungumzii aina hiyo ya mapenzi kabsaaa! Kwani mara nyingi katika aina hii ya mapenzi watu hutamaniana tu kwa maslahi Fulani. Mie nazungumzia mapenzi yatokayo moyoni,yale ambayo mwanamke haambiwi chochote juu ya mwanaume wake,yale mapenzi ambayo katu mwanamke hataki kuona wala kusikia mwanaume wake anateseka wakati yeye yupo na anaweza kumsaidia. Wadada warembo na wanaojiheshimu hakika anapenda wanaume wenyetabia zifuatazo;-

*Mwanaume mwenye kujiamini na mwenye kutumia hekma ya hali ya juu katika kufanya maamuzi yake.Hiki ni kigezo kikubwa sana ambacho maranyingi watoto wakali na wenye kujiheshimu huwa wanakitafuta kwasababu kama hujiamini na busara ni sifuri basi ni rahisi sana kuanza kumtilia wasiwasi na kuhisi lazima unasalitiwa kutokana na uzuri waliojaaliwa. Warembo hawa huwa hawapendi kuwa na watu wenye hasira za karibu kwani wanajua fika kwa urembo walio nao na kwa jinsi wanavyotakwa na maelfu ya wanaume wanaweza wakawa wanapigwa kila uchao kwa sababu ya wivu uliokithiri wa waumezao.

*Hupenda wanaume wenye nidhamu kwa wanawake wengine sio mtu mwenye shobo kwa kila mwanamke kwani kufanya hivyo kunafanya wahisi sio spesho kwako kwani hujamchukulia kama mtu pekee mwenye kustahili vitu spesho. Mrembo mwenye kujithamini na kujiheshimu anafurahi sana pale anapoona mwanaume wake anampa heshima na kumonesha kumjali kwa namna tofauti na mwanamke wa kawaida ambaye si mpenzi wake.

*Mwanaume mchapakazi na mwenye usongo na mafanikio maishani hupendwa sana na aina hii ya wadada kwani kutokana na uzuri wao yaani motto mashallah kwanini jamani athubutu kuwa na jitu ambalo halijishughulishi wala halina mpango wa kutafuta maendeleo kwaajili ya maisha yao badae. Aina hii ya wadada huwa wanaogopa kaka ambae ni muuza sura pekee ambaye si mtafutaji hivyo kama wewe unakaa unabweteka tu na unategemea mambo yanyooke tu kwakweli umelamba reli andikia maumivu kwani hata dada anayejitambua huwezi kumg’oa.

*Mwanaume ambaye hakati tamaa katika harakati zake za kila siku na hata akiwa anamfukuzia aina hii ya mdada anakuwa anaonesha nia ya dhati ya kumhitaji.Hivyo kwa mwanaume yoyote anayetaka vitu vizuri lazima ujipange na sio kutaka tu rahisi rahisi ndio maana wazungu wanamsemo wao usemao “what comes easy goes easy” hivyo hutakiwi kulegeza mtoto wakiume.
#SHARE THIS NEWS AND WIN!!!#

You Might Also Like

0 comments

JIUNGE UPATE HABARI

Jisajili Sasa upate E-mail ya Kila Tunachochapisha....